Mshambulizi wa Kariobangi Sharks na timu ya taifa Harambee Stars, Masoud Juma amejiunga na klabu ya Afrika Kusini Cape Town City. Klabu hiyo ilitangaza usajili huo katika mtandao wao wa Twitter mapema leo. Hata hivyo hela za usajili hazijawekwa wazi. Juma amekuwa nguzo muhimu kwa kikosi cha Harambee…
Mlinzi wa Southampton Virgil Van Djik atajiunga na Liverpool mwezi Januari tarehe moja kwa rekodi ya paundi milioni sabini na tano (£75M). Nyota huyo wa Uholanzi alifaa kujiunga na The Reds mwezi Julai, ila uhamisho huo ukafeli baada ya kujulikana kuwa Liverpool haikufuata sheria katika kutaka kumsajili. Usajili huo…
Mshambulizi wa timu ya taifa ya Uingereza na klabu ya Tottenham Harry Kane, amevunja rekodi ya mabao thelathini na sita iliyowekwa na Alan Shearer miaka ishirini na mbili iliyopita. Shearer alifunga mabao hayo akiwa na klabu ya Blackburn Rovers mwaka wa 1995. Kane alifunga mabao matatu siku ya Jumanne…
Aliyekuwa kiungo mtengenezaji wa Arsenal na Borussia Dortmund, Tomas Rosicky amestaafu. Gwiji huyo aliyependwa sana kwa mchezo wake wa gusa niguse alitangaza kustaafu hiyo jana, katika maongezi na vyombo vya habari kule Jamhuri ya Czech. Rosicky alisema kuwa ameafikia uamuzi huo kwa kuwa umri wake wa miaka 37 haumruhusu…
Aliyekuwa kiungo mshambulizi wa AC Milan na Real Madrid, Ricardo Izecsano dos Santos Leite almaarufu Kaka, ametundika dalugha. Kaka aliandika ujumbe wa kustaafu kwake kwenye ukurasa wake wa Instagram, mapema leo. Nyota huyo amestaafu akiwa na umri wa miaka thelathini na tano, huku akijivunia rekodi nzuri ya…
Timu ya taifa Harambee Stars ndio mabingwa wa kombe la CECAFA mwaka huu baada ya kuicharaza na kuilabua Zanzibar, mabao matatu kwa mawili kwenye fainali. Mechi hiyo iliyogaragazwa kule Machakos, ilizua mchecheto na mhemko si haba, hadi dakika ya mwisho. Kenya ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa…
The Minnows ya Zanzibar imejikatia tikiti ya fainali hii leo, baada ya kuicharaza Uganda Cranes mabao mawili kwa moja. Mechi hiyo iligaragazwa katika uga wa Moi kule Kisumu. Abdulazziz Makame alikuwa wa kwanza kucheka na wavu kwa upande wa Zanzibar kunako dakika ya ishirini na mbili, kabla ya…
Klabu ya Wazito iliyopandishwa daraja majuzi iliishangaza Rangers siku ya Jumanne, baada ya kuirindima bao moja kwa nunge. Mechi hiyo ilisakatwa katika uga wa Moi Sports Centre; Kasarani katika sherehe za Jamhuri. Aliyekuwa mshambulizi wa Tusker John Mabia alifunga bao hilo muhimu baada ya kuingizwa kama nguvu mpya.…
Official Tusker FC FROM: TUSKER FOOTBALL CLUB 8th December, 2017 RE: TUSKER FOOTBALL CLUB TRIALS Tusker FC will be conducting a three day trial exercise aimed at recruiting new players ahead of the team’s 2018 campaign. The player selection and trials will be conducted at the club’s…
Droo ya Kombe la klabu bingwa iliandaliwa leo alasiri huku kipute babu kubwa kikisubiriwa kati ya Real Madrid ya Uhispania na Paris Saint Germain ya Ufaransa. Chelsea ya Uingereza inakabiliwa na mtihani mgumu dhidi ya Barcelona ya Uhispania huku Tottenham ikitifua kivumbi dhidi ya Juventus. Timu ya…

